HAPA KWETU FULL KIYOYOZI
Kivulini kwetu tunataka daima mambo yawe mazuri kama ilivyo hapo juu na si vinginevyo kama inavyoonekana hapa chini.
Kwa taarifa tu, hii ninaitoa kama tahadhari kuwa nyie mawakala wa wahamiaji; mchezo wenu ndiyo mauti kwetu.
Habari tulizonazo ni kuwa Kivulini kwetu wahamiaji haramu wamekuwa wengi kupita kiasi . Hatuna uhakika kama watu wa Uhamiaji wanalijua hili kwa mapana yake ama la, lakini iwe iwavyo, mambo yakiharibika wote tutaingia katika matatizo.
Sasa hivi wahamiaji kutoka nchi jirani na za mbali wamekuwa wakipishana mitaani mpaka wenyewe kwa wenyewe wanaanza kukimbiana; lakini sisi wenyeji wala hatuna wasiwasi; tupo tu tunawagawia huduma zote watakazo. Wapo wengi tu wanaouza matunda kwa baiskeli; wapo wanaouza maua na mapazia; wapowanaojifanya makandarasi; wapo wanaojifanya madaktari; wauza vikombe; wasuka nywele; wasanii; wajasiliamali; na wa aina kadha wa kadha. Sasa hivi kila mgeni anatusifia hapa kwetu kwamba KIVULINI KWETU NI FULL KIYOYOZI. Kwamba hapa shida ni kuingia, lakini ukifika ni kama umeingia peponi; hakuna bugudha.
Kitendawili ninachokiona ni kuwa wageni hawa huja mikono mitupu tena kupitia njia za panya, lakini baada ya kipindi kifupi hustawi kushinda hata wenyeji; na ustawi wao huupata kwa kutumia fulsa hizihizi ambazo wakati mwingine wageni tumeshindwa kuzipata. Ni vipi wanafanikisha mambo yao, hilo nalo neno. Anakuja mhamiaji haramu baada ya miezi miwili anapanda cheo anakuwa mwekezaji.
Kwa sasa sio tatizo sana, lakini baada ya muda watazaliana, watanunua ardhi kwa maekali, wataoa shangazi zetu, na wakiwa wengi wanaanzisha kashkash za kwao hapa Kivulini kwetu, kipindi hicho tumejisahau hata madaraka mengine tumewakabidhi. Mbona sisi kwao hatufanyi hivyo na wala hawatuachii tukajimwaga kama sisi tunavyowaachia. Huu wema kuzidi uwezo tumeutoa wapi.
Nimelazimika kusema msije mkasema sikuwaambia.
No comments:
Post a Comment