Friday, 22 August 2014

BLEKINGI NYUZI

      GARI LAIBIWA KIMAZINGARA



Wandugu wapenzi,

Habari tulizozipata sasa hivi ni kuwa Kivulini kwetu limeibiwa gari Lori aina ya Scania likiwa na shehena yake ya mafuta. Lori hilo liikuwa limeegeshwa katika gereji ya kivulini likisubiri kusafiri kesho kwenda nchi za nje kupeleka mafuta hayo.

Gari hili likiwa mali ya kivulini limekutwa halipo lilipoachwa jana.

Cha kushangaza kuhusiana na kutoweka kwa gari hili ni kuwa magurudumu yake yote yakiwemo na ya spea ambayo yalikuwa yamefungwa katika gari hilo yamekutwa mahali lilipokuwepo gari hilo. Imethibitika kuwa magurudumu hayo yalikuwa ya gari hilo kwa kuwa yalikuwa na alama. Kama kuna aliyechukua gari hilo, basi lazima alikuja na magurudumu yake akabadilisha. Kana kwamba hiyo haitoshi, hata ufunguo wa gari hilo umekutwa juu ya mataili hayo.

Habari zaidi za kuaminika zinasema walinzi watatu waliokuwa wakililinda lori hilo wamekutwa wazima lakini wamelala fofofo; na mpaka tunaingia mitamboni juhudi za kuwaamsha zilikuwa hazijawezekana; hivyo walikuwa bado wamelala. Na hivi tunavyosema wapo hospitali wanaendelea kulala chini ya ulinzi mkali.

Wanakivulini waliokutwa eneo hilo la tukio wanadai kuwa hii ni mara ya kwanza kwa wizi wa aina hiyo kutokea ukitilia maanani kuwa gari hilo lilikuwa ndani ya uzio na katikati ya magari mengine ambayo yalikutwa hayajasogezwa japo hatua moja; lakini nafasi lilipokuwepo gari hilo imeachwa wazi na gari halipo..

Tutaendelea kuwajuza kitakachojiri juu ya tukio hili ambalo kwa hakila si la kawaida.

No comments:

Post a Comment