NGANO ZA KIVULINI
MAKUBWA KIVULINI
Siku moja majirani tulikuwa kivulini tunapunga upepo huku
tukiwa na maongezi ya hapa na pale. Tulikuwa watano; wanawake wawili na wanaume
watatu. Tukiwa hatuna hili wala lile akaja mzee mmoja naye jirani yetu
vilevile. Akatusalimu na kasha anaanzisha mada mpya kabisa. Akasema, hebu tuwe
wakweli na kila mmoja atoe mchango wake kwa moyo wote; mmoja mmoja kila mtu
aseme anawaza nini hapo alipo; nini tatizo lake kubwa ambalo linamla akili.
Kwanza tulitazamana, tukacheka na baadae mmoja wetu kwa jina bwana Juma
Kilobaki akaanza kijieleza:
JUMA KILOBAKI: “Ndugu
zangu, kusema kweli mimi ninalowaza ni kuwa nitajikomboaje katika hii hali.
Kwanza, mwanangu jana karudishwa kutoka shuleni anadaiwa ada sh.300,000/=.
Pili, nimeletewa taarifa kutoka nyumbani kuwa mama mzazi kalazwa hospitali;
hana damu, figo moja haifanyi kazi, na mapafu yamejaa maji; kwenda tu kumuona lazima
niwe na 250,000. Tatu,nilikuwa nimekopa Benki ya Posta kwa kila mwezi kurejesha
sh. 180,000/= na tarehe ya marejesho ilikuwa juzi. Nne, nimepata simu muda sio
mrefu kuwa mama mkwe yuko njiani anakuja kutusalimia; yeye na wajukuu zake
wawili; lakini hapa nilipo senti tano kipande sina…..!”
Tulikuwa kama tumekubaliana; wote tukasema “…du !”. Wa pili
nikawa mimi……nikaanza “ Jana nililetewa taarifa kuwa kuwa watoto wa mjomba(mtu
na dada yake) wamepeana mimba. Mjomba mwenyewe amekwisha pata habari juu ya
suala hilo lakini yupo safari; kesho anarudi. Keshatoa maagizo kuwa asiwakute
watoto hao nyumbani kwake. Mkewe kaja nyumbani analia nimsaidie. Sasa ninawaza
nianzeje.”
Ikaja zamu ya Mama Sakina; yeye akaanza lake “…jamani
mwenzeni nina tatizo. Mkilisikia mnaweza kudhani dogo lakini……leo ni karibu
mwezi lakini amini usiamini kila siku ya mungu nikilala usiku ninamuota mume wa
jirani yangu nimelala nae. Yaani ndoto hiyo imenichosha maana nikiamka nikilala
tena ndoto ni hiyohiyo…sijajua nimelogwa, ama nina jinni ama vipi…..sielewi kwa
kweli”
Aliyefuata alikuwa Eliza. Yeye nae alikuwa na lake. “Mwenzenu
mimi tatizo langu ni ndoa. Kila saa
nawaza huu ni mwaka wa 35 lakini haijatokea hata katika utani mwanamume yoyote
kunitamkia ndoa. Na si ndoa tu hata kuniambia chochote kwamba ananipenda au
nini. Nikijiangalia mwenyewe sijoni kama nina kasoro sasa hii hali mpaka lini.
Msinione ninacheka mkadhani vipi mwenzenu inaniuma kwelikweli sina hata raha na
maisha” Kila mmoja wetu akabaki ameduwaa.
Wa mwisho alikiwa Dick Mbalanga. “ Mwenzenu mimi nasumbuliwa
na mke wangu, siyo siri kwa kweli atanishinda. Huu sasa nikihama utakuwa mtaa
wa tisa ndani ya mwaka mmoja. Mtaa wa kwanza alimpiga baba mwenye nyumba. Mtaa
wa pili alifumaniwa na mume wa jirani yetu. Mtaa wa tatu alikutwa anafukia
hirizi mlangoni kwa mwenye nyumba. Mtaa wanne nikiwa safari alikamata bata wa
watu akamkaanga wakati mimi niliposafiri nilimwachia hela kibao za matumizi.
Mtaa wa tano amekula hela za watu za upatu. Mtaa wa sita kamchoma kisu binti
mmoja jirani, kisa, anamshuku kuwa mimi ninatembea nae. Mtaa wa saba aligombana
na mama mwenye nyumba akachukua mafuta na kiberiti kutaka kuchoma nyumba. Mtaa
wa nane ilibidi nihame maana alikuwa anatembea na mpemba mmoja ayelikuwa na
duka lake nyumba hiyohiyo. Sasa juzi mke wangu kagombana na wapangaji wenzie
akawatishia maisha na wenzake wamemwambia watamfanyizia…….mkumbuke huko kote
hatukukaa tukamaliza mwaka, tulikuwa tunahama tunasamehe kodi miezi iliyobaki.”
Yule jamaa aliyetuhoji akatuangalia kingano za kivulnsha akasema
“….mnaona ndugu zangu, kipindi mnaongea mliyajua haya ?; kazi kwenu mimi
siyawezi labda kivuli kitawasaidia. Akaondoka na kutuacha midomo wazi kivulini.
No comments:
Post a Comment