HAPA KWETU FULL KIYOYOZI
Kivulini kwetu tunataka daima mambo yawe mazuri kama ilivyo hapo juu na si vinginevyo kama inavyoonekana hapa chini.
Kwa taarifa tu, hii ninaitoa kama tahadhari kuwa nyie mawakala wa wahamiaji; mchezo wenu ndiyo mauti kwetu.
Habari tulizonazo ni kuwa Kivulini kwetu wahamiaji haramu wamekuwa wengi kupita kiasi . Hatuna uhakika kama watu wa Uhamiaji wanalijua hili kwa mapana yake ama la, lakini iwe iwavyo, mambo yakiharibika wote tutaingia katika matatizo.
Sasa hivi wahamiaji kutoka nchi jirani na za mbali wamekuwa wakipishana mitaani mpaka wenyewe kwa wenyewe wanaanza kukimbiana; lakini sisi wenyeji wala hatuna wasiwasi; tupo tu tunawagawia huduma zote watakazo. Wapo wengi tu wanaouza matunda kwa baiskeli; wapo wanaouza maua na mapazia; wapowanaojifanya makandarasi; wapo wanaojifanya madaktari; wauza vikombe; wasuka nywele; wasanii; wajasiliamali; na wa aina kadha wa kadha. Sasa hivi kila mgeni anatusifia hapa kwetu kwamba KIVULINI KWETU NI FULL KIYOYOZI. Kwamba hapa shida ni kuingia, lakini ukifika ni kama umeingia peponi; hakuna bugudha.
Kitendawili ninachokiona ni kuwa wageni hawa huja mikono mitupu tena kupitia njia za panya, lakini baada ya kipindi kifupi hustawi kushinda hata wenyeji; na ustawi wao huupata kwa kutumia fulsa hizihizi ambazo wakati mwingine wageni tumeshindwa kuzipata. Ni vipi wanafanikisha mambo yao, hilo nalo neno. Anakuja mhamiaji haramu baada ya miezi miwili anapanda cheo anakuwa mwekezaji.
Kwa sasa sio tatizo sana, lakini baada ya muda watazaliana, watanunua ardhi kwa maekali, wataoa shangazi zetu, na wakiwa wengi wanaanzisha kashkash za kwao hapa Kivulini kwetu, kipindi hicho tumejisahau hata madaraka mengine tumewakabidhi. Mbona sisi kwao hatufanyi hivyo na wala hawatuachii tukajimwaga kama sisi tunavyowaachia. Huu wema kuzidi uwezo tumeutoa wapi.
Nimelazimika kusema msije mkasema sikuwaambia.
Saturday, 30 August 2014
UBINAADAMU KAZI
KWANI SALAMU KILO BEI GANI ?
Kwenu msiopenda kusalimia na kusalimiwa,
Kuvulini kwetu wamenituma niwaambie ama niwapashe mpashike kuwa tabia hii mliyonayo ni chafu na inatia kichefuchefu. Tabia yenyewe ni ya kuwa wazito katika salamu. Kwanza hamna utaratibu wa kusalimia watu na mbaya zaidi hata mkisalimiwa hampokei salamu na kama mnapokea basi ni kama mnalazimishwa. Kwani hamjui kuwa salamu ndiyo kipimo cha awali cha ustaarabu wa mtu ? Basi habari ndiyo hiyo.
Watu wa kivulini kwetu wamewachokeni kwa tabia hiyo ya ovyo. Ikiwa hata mbwa, kuku, nyani na wengineo wakikutana wanasalimiana sembuse wewe mwanadamu usiyekuwa na mkia. Kumbe ubinaadamu wako umekalia wapi; miguuni kiunoni ama kichwani ? Kwa kweli mnaudhi.
Nalisema hil ili liwatue vizuri vichwani mwenu. Ebu tuelezeni, tabia hiyo ni kwa vile mna pesa sana, ama ni kwa vile mmesoma sana ama ni kwa ajili gani. Na mseme pia kama mkiwasalimia watu ama mkiitikia salamu za watu mtapungukiwa nini. Na kama mnajua bei ya salamu huko mnunuako tuelezeni salamu kwa kilo mnauziwa bei gani ? Mbona sisi tunajua salamu hazina gharama.
Utawakuta watu hawana cha pesa, hawana cha elimu, hawana sura nzuri; kwanza miguu yao yote ni ya kushoto lakini mabahili kwa salamu kushinda hata nyoka. Nini hasa kinawasumbua ? Mmelogwa ?
Wenyewe ukiwabana utasikia wanasema kwani salamu ni lazima; kwa taarifa yetu ili mradi nyinyi ni binadamu na tuko nanyi katika jamii hii, salamu ni lazima. Ni lazima kwa sababu hatima yako wewe ni kifo na siku ukifa hatutakuacha barabarani utuozee utunukie; tutalazimika sisi kubana pua zetu kukuzoazoa na kwenda japo kukutupa jalalani; sasa sisi utatulipa nini na kipindi hicho kujitambui. Maiti hazikwi na pesa, hazikwi na vyeti, wala hazikwi madaraka, anazikwa mtupu kama alivyozaliwa; sasa mnalinga nini nyie.
Jambo jingine ni kuwa wewe ni binadamu eti siyo tumbili; na binadamu kama walivyo viumbe wengine tuna taratibu zetu ambazo ni lazima zifuatwe ili tukukubali katika jamii; vinginevyo hamia msituni ukaishi na mafisi wenzio utuache sisi tusalimiane; kwanza hutulishi, hutuvishi na wala wewe sio barabara kusema tutapita wapi.
Ninaongea hivi kwa hasira kutokana na kukerwa. Mtu anakuja msibani anawakuta watu wamejaa, hana salamu hana cha nini anakaa kwenye kiti na kuendelea kubonyezabonyesa kasimu kake ka mchina; hata kuwashika mikono wafiwa anaona tabu; kumbe kilichomleta pale kitu gani. Ama mtu anaingia katika ofisi ya watu hasalimii wala haulizi getini; ili mradi alikwishaongea na mwenyeji wake kuwa atakuja basi. Ama jirani yenu kila siku akiingia au akitoka hasalimii majirani. Hawa ndio wanaosababisha majirani wanafungulia muziki mpaka sauti ya mwisho siku wanaumwa ama wamefiwa katika vyumba vyao.
Hii ni mara yangu ya mwisho kuwakumbusha nyinyi takataka msiojua maana na umuhimu wa salamu; kwamba kuwakumbusha huku si kutaka chochote kutoka kwenu bali ni kuwafahamisha kuwa ubinaadamu kazi hivyo lazima muwajibike kama binaadamu hata kama mlilelewa ndivyo sivyo; salimieni na pokeeni salamu; vinginevyo nendeni mkaishi na majongoo vichakani; mtuondolee kiwingu.
Kwenu msiopenda kusalimia na kusalimiwa,
Kuvulini kwetu wamenituma niwaambie ama niwapashe mpashike kuwa tabia hii mliyonayo ni chafu na inatia kichefuchefu. Tabia yenyewe ni ya kuwa wazito katika salamu. Kwanza hamna utaratibu wa kusalimia watu na mbaya zaidi hata mkisalimiwa hampokei salamu na kama mnapokea basi ni kama mnalazimishwa. Kwani hamjui kuwa salamu ndiyo kipimo cha awali cha ustaarabu wa mtu ? Basi habari ndiyo hiyo.
Watu wa kivulini kwetu wamewachokeni kwa tabia hiyo ya ovyo. Ikiwa hata mbwa, kuku, nyani na wengineo wakikutana wanasalimiana sembuse wewe mwanadamu usiyekuwa na mkia. Kumbe ubinaadamu wako umekalia wapi; miguuni kiunoni ama kichwani ? Kwa kweli mnaudhi.
Nalisema hil ili liwatue vizuri vichwani mwenu. Ebu tuelezeni, tabia hiyo ni kwa vile mna pesa sana, ama ni kwa vile mmesoma sana ama ni kwa ajili gani. Na mseme pia kama mkiwasalimia watu ama mkiitikia salamu za watu mtapungukiwa nini. Na kama mnajua bei ya salamu huko mnunuako tuelezeni salamu kwa kilo mnauziwa bei gani ? Mbona sisi tunajua salamu hazina gharama.
Utawakuta watu hawana cha pesa, hawana cha elimu, hawana sura nzuri; kwanza miguu yao yote ni ya kushoto lakini mabahili kwa salamu kushinda hata nyoka. Nini hasa kinawasumbua ? Mmelogwa ?
Wenyewe ukiwabana utasikia wanasema kwani salamu ni lazima; kwa taarifa yetu ili mradi nyinyi ni binadamu na tuko nanyi katika jamii hii, salamu ni lazima. Ni lazima kwa sababu hatima yako wewe ni kifo na siku ukifa hatutakuacha barabarani utuozee utunukie; tutalazimika sisi kubana pua zetu kukuzoazoa na kwenda japo kukutupa jalalani; sasa sisi utatulipa nini na kipindi hicho kujitambui. Maiti hazikwi na pesa, hazikwi na vyeti, wala hazikwi madaraka, anazikwa mtupu kama alivyozaliwa; sasa mnalinga nini nyie.
Jambo jingine ni kuwa wewe ni binadamu eti siyo tumbili; na binadamu kama walivyo viumbe wengine tuna taratibu zetu ambazo ni lazima zifuatwe ili tukukubali katika jamii; vinginevyo hamia msituni ukaishi na mafisi wenzio utuache sisi tusalimiane; kwanza hutulishi, hutuvishi na wala wewe sio barabara kusema tutapita wapi.
Ninaongea hivi kwa hasira kutokana na kukerwa. Mtu anakuja msibani anawakuta watu wamejaa, hana salamu hana cha nini anakaa kwenye kiti na kuendelea kubonyezabonyesa kasimu kake ka mchina; hata kuwashika mikono wafiwa anaona tabu; kumbe kilichomleta pale kitu gani. Ama mtu anaingia katika ofisi ya watu hasalimii wala haulizi getini; ili mradi alikwishaongea na mwenyeji wake kuwa atakuja basi. Ama jirani yenu kila siku akiingia au akitoka hasalimii majirani. Hawa ndio wanaosababisha majirani wanafungulia muziki mpaka sauti ya mwisho siku wanaumwa ama wamefiwa katika vyumba vyao.
Hii ni mara yangu ya mwisho kuwakumbusha nyinyi takataka msiojua maana na umuhimu wa salamu; kwamba kuwakumbusha huku si kutaka chochote kutoka kwenu bali ni kuwafahamisha kuwa ubinaadamu kazi hivyo lazima muwajibike kama binaadamu hata kama mlilelewa ndivyo sivyo; salimieni na pokeeni salamu; vinginevyo nendeni mkaishi na majongoo vichakani; mtuondolee kiwingu.
Thursday, 28 August 2014
MTAANI KWETU
VALANGATI KIVULINI
Ndugu zangu leo Kivulini kwetu kumetokea valangati la kufa
mtu.
Majira kama ya saa tano asubuhi maeneo ya mtaa wa madukani niliukuta umati wa watu wakishuhudia patashika nguo kuchanika baina ya
akinamama wawili. Vurugu iliyokuwapo pale ilikuwa si ya kuzimwa na wapita njia.
Mungu ashukuliwe baada ya msukosuko mkubwa kwa bahati wakapita askari wa Tigo
na pikipiki lao ndio waliofanikiwa kumaliza kasheshe ile tena baada ya kulipua
kabomu kadogo ka kutoa machozi.
Utulivu uliporejea nikapata fulsa ya kuongea na mmoja wa
mashuhuda waliokuwepo kutoka mwanzo ili nijue chanzo cha kadhia hiyo; ndipo
nilipopewa mkanda mzima.
Chanzo chetu cha habari kinasema kisa cha ugomvi huo ni
mwekezaji wa ndani ambaye ana hotelibaa pale mtaani palipotokea ugomvi.
Inasemekana mwekezaji huyo alikuwa amemwajiri dada mmoja kutoa huduma katika
mradi huo ambaye kutokana na umahiri wake na bidii yake ya kazi akaamua
kumuongeza jukumu la kumhudumia pia yeye mwekezaji binafsi.
Chanzo chetu cha habari kinaendelea kumwaga cheche kwa
kusema kuwa baada ya kipindi kifupi tokea mwekezaji huyo amtunukie shahada
mhudumu wake akatokea mteja mmoja wa kike ambaye naye kutokana na umaarufu
wake katika ile hotelibaa ikapelekea mwekezaji kumtunukia medali ya uteja wa
kutukuka na hivyo mbali ya kuwa mteja katika mradi akawa pia mteja wake
binafsi.
Changanya kanganya hii iliendelea kwa kipindi cha kama mwezi
mmoja hivi bila mteja bora na mhudumu mahiri kutambuana kuwa wapo katika
kujenga nyumba moja. Wenyewe wakawa wanacheka na kuchangamkiana sana kiasi cha
kuwa mashosti. Lakini wapo baadhi ya wateja na wahudumu katika kiwekezwa hicho ambao walikuwa wanajua
kuwa urafiki huo ulikuwa ni wa mashaka; kwamba walikuwa wakila sahani moja bila wenyewe kugusana mikono.
Kikichotokea leo ni kama ajali. Ilikuwa ni kawaida kwa
mwekezaji kumpa kinoti kama kibali mteja bora kumpelekea mhudumu mahiri ili apewe huduma aliyokuwa anaitaka na pesa
atalipa atakapojisikia. Kwa bahati mbaya leo aliandika vinoti viwili; kimoja
cha huduma kwa mteja na kingine cha huduma kwa mwekezaji; vikiwa katika karatasi
zinazofanana. Kwa uzembe wa mteja bora alipofika kwa shosti wake akajichanganya
na kutoa kinoti cha huduma binafsi ya mwekezaji ambamo ndani ya kinoti hicho
kulikuwa na jina la mteja bora lililoanza na haneei, likifuatiwa na saa ya kukutana, mahali pa kukutana, nini cha
kufanya na mambo mengine ambayo hayaandikiki na chini ya kinoti hicho kulitiwa
saini kwa mbwembwe na mwekezaji mwenyewe.
Mhudumu mahiri baada ya kupokea kinoti hicho kwa makosa na yeye
akakosea kumhoji kwa kumuuliza mteja bora ana maana gani kumpatia ujumbe ambao si wake ama
ndiyo kantangaze anaianzia kwake. Mteja bila kengere kogonga kichwani kwake
akahoji kuwa kama ujumbe haumuhusu maneno yote hayo yanakujaje; kwani inahuu..
Majibizano yakiwa katika hatua za awali, mara akaingia
mwekezaji pale hotelibaa; kuingia kwake ikawa kama unazima moto kwa kupulizia
gesi asilia. Yakaanza kurushwa maneno, jembe, matusi, vitisho, kutoka pembe
hadi pembe; aliyekuwa na masikio ya chuma alisikiliza na mwenye masikio ya mbao
alisalimisha masikio yake maana matusi
na kashfa zilizokuwa zikimwagwa pale zilikuwa ni mpya kutoka dukani ambazo zilikuwa hazijawahi kutumika.
Kana kwamba hiyo haitoshi vitendea kazi na bidhaa zikaanza kutumika kama
silaha za mapambano na ukumbi wote wa biashara ukawa mbengelembengele; vurumai hadi barabarani. Ilibidi ili
kujenga heshima mwekezaji aingie mitini na kuacha gari liende bila dereva maana mambo sasa yalikuwa si mambo.
Baada ya kupata taarifa hiyo nikabaki ninajiuliza kufanya
vurugu kiasi hiki wale akina dada mashosti wakati wote ni madoezi maana yake nini
na yule mwenye mali aliyeko nyumbani afanyeje ? Na huyu mwekezaji naye huu ndio kweli
utaratibu wa kuwekeza; kwa kuwa na mhudumu mpaka binafsi na mteja mpaka binafsi.
Kwa staili hii uchumi kivulini kwetu utaimarika kweli ?
Wednesday, 27 August 2014
BARUA PEPE KWENDA USTAWI WA JAMII
WATOTO WA MITAANI NA WALALA MATANGA
Kwenu Waheshimiwa sana Wana Ustawi wa jamii,
Jamii ya Kivulini kwetu imelazimika kutuma barua hii pepe ipeperuke hadi ije kuwapepea enyi waheshimiwa sana ambao kwa hakika tunawategemea.
Madhumuni ya waraka huu ni kuwazindua mkumbuke shuka kabla usingizi haujawakolea na pia kabla ya usiku wa manane ili msijekumbuka shuka wakati kumekucha.
Mara tu baada ya kupokea waraka huu ebu kwa mchana pitieni kwenye makutano yote ya barabara muone jinsi ustawi unavyomomonyoka na kuzorota. Mtajionea jinsi ambavyo wananchi wa kila rika walivyogeuza makutano ya barabara na bustani za miji kuwa makazi rasmi na ya kudumu. Wameweka majiko ya kupikia, fenicha za kukalia na kulalia. Wanafua, wanapika, wanapiga soga na mengine mengi ya kinyumbani yanaendelea.
Baada ya hapo ebu nyakati za usiku piteni mitaa ya masoko muone jinsi ambavyo watu wamelala kuanzia mwanzo wa mitaa hadi inakoishia utadhani kuna misiba iliyounganika mtaa mmoja hadi mwingine.
Yawezekana waheshimiwa mmebanwa na kazi za kuingiza data maofisini; lakini ebu fanyeni mtoke ofisini muende kwenye kwenye viwanja ili mpate kuona jinsi jamii inavyopoteza mwelekeo. Kitendo cha watu milioni kulala nje lazima kuna namna mahali hapajakaa vizuri. Nina uhakika Waziri wa Makazi na Nyumba hajachacha kiasi hicho na wala hajui kuna watu wengi kiasi hicho wanalala nje.
Vinginevyo tuvunje Wizara ya Ustawi tuunde kitu kingine kitakachosaidia kustawisha jamii maana hali kwa kweli ni mbaya na inatisha. Watu wanakutwa wanakoroma barabarani mpaka saa mbili....kwao wapi ?
Kwenu Waheshimiwa sana Wana Ustawi wa jamii,
Jamii ya Kivulini kwetu imelazimika kutuma barua hii pepe ipeperuke hadi ije kuwapepea enyi waheshimiwa sana ambao kwa hakika tunawategemea.
Madhumuni ya waraka huu ni kuwazindua mkumbuke shuka kabla usingizi haujawakolea na pia kabla ya usiku wa manane ili msijekumbuka shuka wakati kumekucha.
Mara tu baada ya kupokea waraka huu ebu kwa mchana pitieni kwenye makutano yote ya barabara muone jinsi ustawi unavyomomonyoka na kuzorota. Mtajionea jinsi ambavyo wananchi wa kila rika walivyogeuza makutano ya barabara na bustani za miji kuwa makazi rasmi na ya kudumu. Wameweka majiko ya kupikia, fenicha za kukalia na kulalia. Wanafua, wanapika, wanapiga soga na mengine mengi ya kinyumbani yanaendelea.
Baada ya hapo ebu nyakati za usiku piteni mitaa ya masoko muone jinsi ambavyo watu wamelala kuanzia mwanzo wa mitaa hadi inakoishia utadhani kuna misiba iliyounganika mtaa mmoja hadi mwingine.
Yawezekana waheshimiwa mmebanwa na kazi za kuingiza data maofisini; lakini ebu fanyeni mtoke ofisini muende kwenye kwenye viwanja ili mpate kuona jinsi jamii inavyopoteza mwelekeo. Kitendo cha watu milioni kulala nje lazima kuna namna mahali hapajakaa vizuri. Nina uhakika Waziri wa Makazi na Nyumba hajachacha kiasi hicho na wala hajui kuna watu wengi kiasi hicho wanalala nje.
Vinginevyo tuvunje Wizara ya Ustawi tuunde kitu kingine kitakachosaidia kustawisha jamii maana hali kwa kweli ni mbaya na inatisha. Watu wanakutwa wanakoroma barabarani mpaka saa mbili....kwao wapi ?
Monday, 25 August 2014
NGANO ZA KALE
HEKAYA ZA SUNGURA
Ipo hadithi moja ambayo wengi wetu hatuijui yote bali tunaijua kipande tu; hadithi hii ni ya Sungura mjanja na ndizi mbichi.
Inasemekana kuwa hapo zamani za kale SUNGURA mjanja alikwenda kondeni ambako kulikuwa na migomba ambayo mingi kati yake ilikuwa imebeba mikungu ya ndizi.
Siku hiyo ambayo Sungura aliingia katika shamba hilo alikuwa na njaa sana lakini kwa bahati mbaya mikungu karibu yote ilisheheni ndizi zilizokuwa mbichi japo zilikuwa zimekomaa.
Kutokana na njaa aliyokuwa nayo akaona ni heri ajaribu kufanya maarifa apate japo ndizi kadhaa chache aweze kutuliza njaa yake na ikiwezekana kiasi apelekee wanae. Kwa kutumia nguvu zilizokuwa zimebaki mwilini mwake akatikisa kila mgomba ili aweze kupata chochote; lakini bahati haikuwa yake; hakuna hata ndizi moja iliyoanguka; alichoambulia ni uchovu zaidi.
Baada ya Sungura kuona mambo yameshindikana akaamua kutoka kwa hasira huku akisema SIZITAKI.....MBICHI HIZI. Wakati akiyasema hayo Sungura hakujua kuwa hakuwa peke yake katika lile shamba; alikuwepo SHORE pia. Shore alimwonea huruma sana sungura kwa namna alivyochoka na kunyong'onyea kwa njaa kiasi cha kutembea kwa shida kuelekea kwao. Hakumsemesha hata neno moja akamwacha aende zake.
Baada ya siku mbili karibu shamba zima la migomba ndizi zote ziliiva. Kwa kuwa Shore alikuwa habanduki shambani hata kama ndizi ni mbichi; kwa kuona zimeiva akamkumbuka Sungura. Akaamua akamwite aje shamba ale kwa kadri atakavyoweza.
Kwa bahati Shore akamkuta Sungura maskani kwake akamwomba wafuatane kwenda shamba. Sungura mwanzoni alikataa katakata kuwa yeye hana haja ya ndizi kwanza ndizi zenyewe mbichi. Lakini baada ya kubembelezwa sana akaamua aongozane na Shore kwenda shambani.
Walipofika shambani Sungura hakuamini macho yake kwani ndizi zote zilikuwa zimebadilika rangi. Shore akamwambia Sungura aanze kutikisa migomba. Katika kutikisa mgomba wa kwanza tu zilidondoka ndizi ambazo kwa siku ile Sungura na familia yake hawangeweza kuzimaliza.
Akiwa mwenye furaha Sungura akamwuliza Shore kuwa amejuaje kuwa ndizi zile zilikuwa zimeiva. Shore akamwambia kuwa yeye huwa habanduki shambani hata kama ndizi mbivu zimeisha bali hukaa humo humo shambani akila matunda mengine hadi ndizi mbichi zinaiva. Hapo ndipo Sungura alipomwangalia Shore kwa mshangao na kutikisa kichwa huku akisema " ama kweli MVUMILIVU HULA MBIVU".
Ipo hadithi moja ambayo wengi wetu hatuijui yote bali tunaijua kipande tu; hadithi hii ni ya Sungura mjanja na ndizi mbichi.
Inasemekana kuwa hapo zamani za kale SUNGURA mjanja alikwenda kondeni ambako kulikuwa na migomba ambayo mingi kati yake ilikuwa imebeba mikungu ya ndizi.
Siku hiyo ambayo Sungura aliingia katika shamba hilo alikuwa na njaa sana lakini kwa bahati mbaya mikungu karibu yote ilisheheni ndizi zilizokuwa mbichi japo zilikuwa zimekomaa.
Kutokana na njaa aliyokuwa nayo akaona ni heri ajaribu kufanya maarifa apate japo ndizi kadhaa chache aweze kutuliza njaa yake na ikiwezekana kiasi apelekee wanae. Kwa kutumia nguvu zilizokuwa zimebaki mwilini mwake akatikisa kila mgomba ili aweze kupata chochote; lakini bahati haikuwa yake; hakuna hata ndizi moja iliyoanguka; alichoambulia ni uchovu zaidi.
Baada ya Sungura kuona mambo yameshindikana akaamua kutoka kwa hasira huku akisema SIZITAKI.....MBICHI HIZI. Wakati akiyasema hayo Sungura hakujua kuwa hakuwa peke yake katika lile shamba; alikuwepo SHORE pia. Shore alimwonea huruma sana sungura kwa namna alivyochoka na kunyong'onyea kwa njaa kiasi cha kutembea kwa shida kuelekea kwao. Hakumsemesha hata neno moja akamwacha aende zake.
Baada ya siku mbili karibu shamba zima la migomba ndizi zote ziliiva. Kwa kuwa Shore alikuwa habanduki shambani hata kama ndizi ni mbichi; kwa kuona zimeiva akamkumbuka Sungura. Akaamua akamwite aje shamba ale kwa kadri atakavyoweza.
Kwa bahati Shore akamkuta Sungura maskani kwake akamwomba wafuatane kwenda shamba. Sungura mwanzoni alikataa katakata kuwa yeye hana haja ya ndizi kwanza ndizi zenyewe mbichi. Lakini baada ya kubembelezwa sana akaamua aongozane na Shore kwenda shambani.
Walipofika shambani Sungura hakuamini macho yake kwani ndizi zote zilikuwa zimebadilika rangi. Shore akamwambia Sungura aanze kutikisa migomba. Katika kutikisa mgomba wa kwanza tu zilidondoka ndizi ambazo kwa siku ile Sungura na familia yake hawangeweza kuzimaliza.
Akiwa mwenye furaha Sungura akamwuliza Shore kuwa amejuaje kuwa ndizi zile zilikuwa zimeiva. Shore akamwambia kuwa yeye huwa habanduki shambani hata kama ndizi mbivu zimeisha bali hukaa humo humo shambani akila matunda mengine hadi ndizi mbichi zinaiva. Hapo ndipo Sungura alipomwangalia Shore kwa mshangao na kutikisa kichwa huku akisema " ama kweli MVUMILIVU HULA MBIVU".
Saturday, 23 August 2014
KIPEPERUSHI
UJUMBE KUTOKA KWA MFADHIRI
Leo Kivulini tumetumiwa kipeperushi chenye ujumbe mzito kutoka kwa mwekezaji. Amesema tukisome na kama kitafaa tukipeleke kwa waheshimiwa wakae nacho kama akiba kwani siku zote akiba haiozi. Japo Kivulini si uwanja wa siasa lakini ukweli ni kwamba hakuna maisha yasiyo na siasa. Tunaomba kuwasilisha kipeperushi hicho. Asanteni sana.
Leo Kivulini tumetumiwa kipeperushi chenye ujumbe mzito kutoka kwa mwekezaji. Amesema tukisome na kama kitafaa tukipeleke kwa waheshimiwa wakae nacho kama akiba kwani siku zote akiba haiozi. Japo Kivulini si uwanja wa siasa lakini ukweli ni kwamba hakuna maisha yasiyo na siasa. Tunaomba kuwasilisha kipeperushi hicho. Asanteni sana.
Friday, 22 August 2014
BLEKINGI NYUZI
GARI LAIBIWA KIMAZINGARA
Wandugu wapenzi,
Habari tulizozipata sasa hivi ni kuwa Kivulini kwetu limeibiwa gari Lori aina ya Scania likiwa na shehena yake ya mafuta. Lori hilo liikuwa limeegeshwa katika gereji ya kivulini likisubiri kusafiri kesho kwenda nchi za nje kupeleka mafuta hayo.
Gari hili likiwa mali ya kivulini limekutwa halipo lilipoachwa jana.
Cha kushangaza kuhusiana na kutoweka kwa gari hili ni kuwa magurudumu yake yote yakiwemo na ya spea ambayo yalikuwa yamefungwa katika gari hilo yamekutwa mahali lilipokuwepo gari hilo. Imethibitika kuwa magurudumu hayo yalikuwa ya gari hilo kwa kuwa yalikuwa na alama. Kama kuna aliyechukua gari hilo, basi lazima alikuja na magurudumu yake akabadilisha. Kana kwamba hiyo haitoshi, hata ufunguo wa gari hilo umekutwa juu ya mataili hayo.
Habari zaidi za kuaminika zinasema walinzi watatu waliokuwa wakililinda lori hilo wamekutwa wazima lakini wamelala fofofo; na mpaka tunaingia mitamboni juhudi za kuwaamsha zilikuwa hazijawezekana; hivyo walikuwa bado wamelala. Na hivi tunavyosema wapo hospitali wanaendelea kulala chini ya ulinzi mkali.
Wanakivulini waliokutwa eneo hilo la tukio wanadai kuwa hii ni mara ya kwanza kwa wizi wa aina hiyo kutokea ukitilia maanani kuwa gari hilo lilikuwa ndani ya uzio na katikati ya magari mengine ambayo yalikutwa hayajasogezwa japo hatua moja; lakini nafasi lilipokuwepo gari hilo imeachwa wazi na gari halipo..
Tutaendelea kuwajuza kitakachojiri juu ya tukio hili ambalo kwa hakila si la kawaida.
Wandugu wapenzi,
Habari tulizozipata sasa hivi ni kuwa Kivulini kwetu limeibiwa gari Lori aina ya Scania likiwa na shehena yake ya mafuta. Lori hilo liikuwa limeegeshwa katika gereji ya kivulini likisubiri kusafiri kesho kwenda nchi za nje kupeleka mafuta hayo.
Gari hili likiwa mali ya kivulini limekutwa halipo lilipoachwa jana.
Cha kushangaza kuhusiana na kutoweka kwa gari hili ni kuwa magurudumu yake yote yakiwemo na ya spea ambayo yalikuwa yamefungwa katika gari hilo yamekutwa mahali lilipokuwepo gari hilo. Imethibitika kuwa magurudumu hayo yalikuwa ya gari hilo kwa kuwa yalikuwa na alama. Kama kuna aliyechukua gari hilo, basi lazima alikuja na magurudumu yake akabadilisha. Kana kwamba hiyo haitoshi, hata ufunguo wa gari hilo umekutwa juu ya mataili hayo.
Habari zaidi za kuaminika zinasema walinzi watatu waliokuwa wakililinda lori hilo wamekutwa wazima lakini wamelala fofofo; na mpaka tunaingia mitamboni juhudi za kuwaamsha zilikuwa hazijawezekana; hivyo walikuwa bado wamelala. Na hivi tunavyosema wapo hospitali wanaendelea kulala chini ya ulinzi mkali.
Wanakivulini waliokutwa eneo hilo la tukio wanadai kuwa hii ni mara ya kwanza kwa wizi wa aina hiyo kutokea ukitilia maanani kuwa gari hilo lilikuwa ndani ya uzio na katikati ya magari mengine ambayo yalikutwa hayajasogezwa japo hatua moja; lakini nafasi lilipokuwepo gari hilo imeachwa wazi na gari halipo..
Tutaendelea kuwajuza kitakachojiri juu ya tukio hili ambalo kwa hakila si la kawaida.
MGENI NJOO MWENYEJI APONE
MGENI KUTOKA MAJUU
Jana
tumepata bahati ya kutembelewa na mgeni kutoka ng’ambo. Mgeni huyu aliwasiri
kivulini kwetu akiwa na maoni kadhaa kwenye mkoba wake kama zawadi badala ya vitu ambavyo
tumevizoea kuletewa na wageni wa aina hii.
Kwanza
mgeni huyu alitupongeza kwa kuunda chombo cha mawasiliano cha kisasa(blog)
kwa madai kuwa angalau tunaonyesha upeo fulani wa maendeleo kwa kwenda na
wakati.
Akiwa
kivulini kwetu alituomba tuendeleze mawasiliano na watu wa mataifa mbalimbali kutumia blog
hiyo kwani dunia ya leo ni kama kijiji; na tujitahidi kuweka mambo ya msingi badala ya kuijaza matusi na uchafu
kama zilivyo blog nyingine nyingi.
Baada
ya kutuasa hivyo alitupatia ujumbe toka umoja wa mabloga wa kwao kuwa sisi wa
kivulini kwa faida yetu na ya vitukuu wetu tuzingatie yafuatayo:
1.
Tujitahidi kuanzia sasa kupunguza kasi ya kuzaliana; tusisubiri maji yakiwa
shingoni ndipo tuweke sheria kalikali. Amedai kuwa ardhi hii tunayoiona kubwa
haitakuwa hivi baada ya miaka kumi ijayo kama matumizi yenyewe yatakuwa kwa
kufuja kama ilivyo sasa. Kingine kitakachotuumbua ni huduma za jamii; kwamba
wao kwao pamoja na maendeleo waliyonayo katika aina mbalibali ya huduma za majii bado kuzaa zaidi ya watoto wawili
katika familia ni kama ajali; labda mama ajaliwe kujifungua mapacha watatu.
Tukumbuke watoto wazaliwapo wanahitaji chakula, matibabu, nguo, elimu na mambo
mengi sana hivyo kuzaa bila mpango si busara. Kila mwanakivuli atoe busati, badala yake aweke nyota ya
kijani mlangoni kwake.
2.
Tupunguze siasa tufanye kazi. Ameshangazwa sana alipowasili kivulini na kumkuta kila mwanakivuli ni
mwanasiasa, mwanaharakati na mwanasheria. Alishangaa kuona kivuli duni kama chetu kina wanaharakati wengi kushinda wataalam wa fani mbalimbali. Ameshangaa kuona tunapoteza muda mwingi sana
kuongea, kushitakiana, kubishana, kulaumiana, na kujadiliana mambo mengi sana ambayo wala hayana tija wala
umuhimu; tena tunayafanya tukiwa katika makundi huku tukimwaga mapesa mengi kupata muafaka . Yeye alisema ipo haja ikibidi tupange siku maalum
za longolongo ziwe japo siku mbili kwa wiki
na siku tano zilizobaki kusiwe na vikao, mikutano, vijiwe wala mabonanza
tujikite katika kazi. Yeye amedai kuwa hakuna kokote walikopata maendeleo kwa
maneno bali kwa kazi. Ametishika sana kukuta robo ya wanakivuli ndio wanaofanya
kazi na robo tatu yote ni wategemezi. Tumesahau hata msemo mtakatifu usemao "ASIYEFANYA KAZI NA ASILE".
3.
Tatu, alitusihi kuwa wazalendo. Ameshangaa kutuona watu wa kivulini
pamoja na matatizo yetu hatujipendi wenyewe na baya zaidi hatupendani. Alishangaa sana kumsikia kijana
wetu mmoja tena msomi aliyesomeshwa na serikali akitamka hadharani bila kujali kazungukwa na nani anasema kwamba anajuta kuzaliwa
kivulini; eti ni heri angelizaliwa mbwa
majuu angeliishi kwa raha sana. Anadai tamko la aina hii kule kwao mtu huyu
angelipigwa risasi kwani hana faida na tena ni sumu katika jamii. Kama ni kwenye kompyuta hiki kingelikuwa kirusi hatari sana. Amedai kuwa
bila ya uzalendo sera nzuri, katiba bora na mipango mizuri havitaweza kutusadia
chochote. Ni lazima turingie kivuli chetu.
4.
Jambo jingine; alitusihi watu wa kivulini tuwe waadirifu
na hasa viongozi. Ameshangaa jinsi ambavyo hatushangai wala kuhoji maajabu ya
kiuchumi yaliyopo kivulini. Kwamba tumeamua kutohoji chochote wala kuwianisha kazi ya mtu na
kipato chake. Kwamba si ajabu tarishi wa mahakama kumiliki gari ya vogi.
Haitushangazi mtoto wa kazi kuwa na jumba la kifahari kijijini kwao. Ni kitu
cha kawaida waziri kumiliki ardhi ya wilaya nzima kwa ajili ya kilimo cha
familia yake. Mwanafunzi kumiliki simu ya milioni na zaidi ni kawaida. Amedai
kwa mwendo huu tuna kama miaka mitano tu iliyobaki maisha kivulini
yasiwezekane. Kundi la walionacho limezidi kuwa dogo mno likiishi katika msongo wa maisha magumu yasiyo na matumaini hata chembe; wakati huohuo kuna kundi dogo linaloishi kama liko mbunguni; linaishi kadri linavyowaza. Amedai kuwa hii
inaongeza chuki na hasira za kundi kubwa; na inavyoonekana muda si mrefu
uvumlivu wa wengi utatoweka watajichukulia vyao walivyoporwa na wachache.
5.
Mgeni huyu amewasilisha mshangao kutoka majuu kuwa kivulini mungu
katujalia kwa kutupa kila kitu ambacho wenzetu wamepewa kimoja kimoja au viwili
ama hawakupata kabisa. Kasema tumepewa bahari, mito, maziwa, wanyama, ardhi,
madini, maajabu, na vingine vingi. Anadai bado anatafiti kuona wapi lilipo
tatizo kiasi cha sisi kushindwa kuongoza kwa utajiri duniani. Amediriki hata
kusema kuwa pengine mataifa kakubwa yanatufanyia chumaulete kutuibia uchumi
wetu kwa mazingira ama tumepigwa kipapai au tumekanyaga mdudu. Amedai lazima rasilimali zetu zitunufaishe wenyewe kwanza sio tunagawa kama njugu ili mradi tu ziishe.
6.
Mwisho ametuonya tusichezee amani tuliyonayo. Ameshauri kila mwenye
kuleta chokochoko tumpe skolashipu aende kusoma digrii ya amani Somalia, Misri,
Parestina au Zaire ili akirejea
afundishe wengine. Amesema maeneo hayo kuna vyuo vizuri sana vya amani; hivyo ni vema vijana wetu tuwaendeleze katika fani hiyo pia.
Baada ya kutupa salamu hizo akatukabidhi zawadi ya
msalaba mwekundu akaondoka.
Thursday, 21 August 2014
METHALI MPYA ZA LEOLEO
CHAGUA MOJA TU......NIKUUZIE
1. Ujanja wa nyani porini, mjini hata kuvuka
barabara hawezi.
2. Panga lake kupangua, kupanga si la upanga
3. Maji yakijaa chupa ndiyo mwisho wa kujaza.
4. Udi haulumbani na ubani.
5. Kioo hakina ila, ila ajitezamaye
6. Mchawi usiku, mchana mganga
1. Ujanja wa nyani porini, mjini hata kuvuka
barabara hawezi.
2. Panga lake kupangua, kupanga si la upanga
3. Maji yakijaa chupa ndiyo mwisho wa kujaza.
4. Udi haulumbani na ubani.
5. Kioo hakina ila, ila ajitezamaye
6. Mchawi usiku, mchana mganga
Wednesday, 20 August 2014
Friday, 15 August 2014
KWANI KUVAA KUNA KAZI ?
BONANZA KIVULINI
Jana Kivulini kulikuwa na Bonanza. Wenyewe wanasema hilo
Bonanza ni tamasha la aina yake ambalo hujumuisha burudani na michezo ya aina
mbalimbali. Kama mjuavyo hayo ni moja ya marupurupu ya kuwa na amani nchini. Watafiti wanadai kuwa
huwezi kukuta mabonanza kwa Waparestina
na wengine ambao kila uchao huna uhakika kama kesho utakuwepo.
Tamasha hilo kwa kweli lilifana sana. Vijana waliitikia
vilivyo wakacheza, wakala mpaka wakanywa.
Kilichoninikwaza mimi,na pengine na wenzangu wengi ni
matumizi mabaya ya bonanza hilo, hasa kwa upande wa vijana. Nilishangazwa sana
kuona namna walivyokuja kivulini bila ya kujistiri maungo yao; hususani akina
dada. Wengi walikuja wamevaa vipande vya nguo na kuacha sehemu muhimu za maungo
yao bila ya kufunikwa.Mungu bariki kumbe vijana wa siku hizi si wakware wala wabakaji.
Labda unaweza kusema nguo za michezo
ndivyo zilivyo. Lakini si hivyo. Mimi jezi nazijua. Zile hazikuwa jezi bali ni
nguo zao za nyumbani. Sikuweza kuelewa vizuri kama hivyo walivyokuja kivulini
ndivyo walivyotoka majumbani kwao ama la. Lakini kubwa ni swali ambalo
nilijiuliza mpaka leo sijapata jibu kuwa akina dada hawa kutujia vile walikuwa
wanataka tuelewe vipi ama walikusudia kutuonyesha nini ? Ninachelea kusema hata
vipande hivyo walivyovaa walikuwa wakiogopa Dola; vinginevyo wanavyoonekana
wangelikuja kama walivyozaliwa kwani walikuwa wamebakiza padogo sana.
Na akina kaka nao sikuwaelewa. Wengi walivalia sarawali zao
nusu ya vikalio na kuacha ngua zao za ndani zikionekana. Kana kwamba hilo
halitoshi wengi walikuwa wametengeneza nywele na kuvaa vidani kiasi kwamba
ilikuwa wakati mwingine vigumu kumtofautisha mtu na dada yake. Hawa nao
walikuwa na ajenda gani kutufanyia vile ?
Yawezekana mwanakivuli mimi nimepitwa na wakati. Na iwe
hivyo; ila kusema kweli vijana hawa ni wazi nao wamepitiwa na wakati; wakati
unawaburuta mzobemzobe kuwapeleka ambako wala hawakujui. Hivi kwa utaratibu huo
wa kuparaganya maumbile, si tunazikonyeza Sodoma na Gomora nyingine ?
Wazazi wapendwa, waalimu, wanazuoni, na viongozi wa dini ebu
saidieni kizazi hiki; sijui kama wanaharakati na hili mnahusika au nyinyi ni
katika siasa, katiba na sera za serikali. Tusaidiane katika kazi hii nzito.
Kwa ushahidi zaidi nawaalikeni wote mje katika Bonanza
kivulini tarehe kama ya jana kuanzia saa 12 asubuhi hadi saa moja usiku katika
viwanja vyetu vilevile mje mjionee vimbwanga vya dijitali.
Subscribe to:
Posts (Atom)