FAIDA YA KIVULINI
Siku zote ukitaka kujua faida ya kivulini ni vema mwenyewe ukaenda kivulini ukajionee mwenyewe. Kwa kusimuliwa wakati mwingine unaweza kudanganywa ama ukaelezwa ukweli na ambaye ana mtazamo tofauti na wako. Kwa mfano, azengewaye na homa; kivulini hupachukia kwani hujisikia baridi. Mchovu hujisikia usingizi na mwenye vibichi kivuli humchelewesha kukausha. Iwe iwavyo kivulini ni patulivu na humliwaza mwenye kuhitaji kuliwazwa; mwenye lake jambo kivulini hupakimbia.
No comments:
Post a Comment