MAMBO YA KIVULINI
Kama ilivyo ada; penye
wema ubaya huwa haukai mbali. Vivyo
hivyo na kivulini, daima huwa hapakosi matatizo. Kwanza kabisa unapokuwa
kivulini lazima ujiandae na kuhama au kusogeasogea; kwani kivuli mara nyingi hutegemea
jua. Tangu kuchomoza jua hadi kuchwa kivuli hutembea au kusogea eneo jipya.
Jambo jingine ni kuwa
kama wewe mwanadamu upendavyo kivuli na viumbe wengine nao hupenda kivuli.
Kivulini waweza kutembelewa na wadudu ama nyoka ambao huwa hawaji kwa ajili
yako, bali hufuata kivuli waweze kujipumzisha pia. Na si hao tu wanaweza pia
kuja wanyama kama simba chui, nyani na wengineo kutegemea kivuli hicho kiko
wapi.
Nasikia pia kivulini
waweza tenmbelewa na viumbe wa ajabu kama majini, mizimu na wengine wa aina
hiyo ambao hupendelea sehemu tulivu ama hutafuta watu watulivu. Iwe iwavyo
kivulini ni mahali penye faraja ili mradi uwapo kivulini kuwa na tahadhari;
lolote linaweza kutokea.